Mitandao

TUICO YAENDESHA MAFUNZO KWA VIJANA KATIKA KUADHIMISHA SIKU YA WAFANYAKAZI 2019

Wafanyakazi Vijana kutoka katika Taasisi Mbalimbali wakiwa katika Semina ya Chimbuko la Vyama, Jijini Mbeya

Chama Cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha Huduma na Ushauri kwa kushirikiana na taasisi ya Public Server International (PSI), kimeendesha semina ya sheria za kazi na Chimbuko la vyama vya wafanyakazi kwa wafanyakazi vijana kutoka katika taasisi na makampuni mbali mbali jijini mbeya.

Semina hiyo iliyohusisha pamoja na mambo mengine, kuwajenga wafanyakazi vijana uwezo wa kuzitambua haki zao kazini pamoja na chimbuko la vyama vya wafanyakazi duniani iliendehswa katika chuo cha wafanyakazi Mbeya maarufu kama 'Chuo cha TUCTA' kilichopo Mwanjelwa Jijini Mbeya. 

Waziri wa Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu,
Mhe. Anthony Mavunde katika picha na washiriki
Mafunzo hayo yalifunguliwa rasmi na Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Mhe. Anthony Mavunde. Katika ufunguzi, Mhe. Mavude alikipongeza Chama Cha TUICO kwa kuonesha njia hata katika vyama vingine kuiga utoaji wa semina kwa wanachama wake. Aliwahasa wafanyakazi kuzingatia sheria za kazi na kujituma ili kujikwamua kiuchumi has tunapoelekea Tanzania ya Viwanda. 

Mwakilishi wa vijana katika mafunzo hayo Bi. Pendo Simbeye (27) ambaye ni mfanyakazi katika sekta ya Viwanda kutoka katika kampuni ya TBL tawi la Mbeya, alikishukuru Chama Cha Wafanyakazi TUICO kwa kuwapa semina hiyo na kukiri kuwa wafanyakazi wengi vijana hawana elimu ya kutosha juu ya haki za msingi za wafanyakazi.

Washiriki wa Semina wakiwa katika mafunzo
Kwa Upande wake, Mwezeshaji katika Semina hiyo kutoka TUICO makao Makuu, Ndugu Sikunzi John, alisema mafunzo haya yamekuwa yakitolea kila mara kwa wafanyakazi wa kada mbali mbali na makundi tofauti tofauti. Aliongeza kuwa lengo hasa la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo wafanyakazi wa kujiamini na kufanya kazi kwa misingi ya sheria na utawala bora.

Mwezeshaji wa Semina ya Chimbuko la Vyama, Ndugu Shikunzi John akielezea jambo wakati wa Semina

Aidha, mkuu wa chuo hicho cha wafanyakazi chenye maskani yake jijini mbeya, Ndugu Edwin Richard Mwakyembe, alikipongeza Chama Cha TUICO na kusema kuwa kwa mtizamo wake TUICO ndio chama cha wafanyakazi pekee nchini Tanzania kinachotekeleza majukumu yake kwa wanachama wake kwa kuwa na watendaji wenye weledi na wabunifu. Aliwahasa wafanyakazi walioko katika sekta zinazohudumiwa na chama cha TUICO kujiunga haraka kwani UMOJA ni Nguvu.

Na: Sebastian Gentanyi
TUICO Makao Makuu


Related

HABARI KUU 8090088779034562341

Post a Comment

emo-but-icon

BSC I SEM II DRAFT II TIMETABLE


Ruaha Catholic University

RUCO MIRROR 2014 EDITION

Almanac 2015/2016

Our Facebook Page

.

Portal Admin


ADVERTISEMENTS

soccer league tables

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Our Recent Visitors

item