JPM, VIMILIA NILALAPO MBELE NA WEWE, HAPA KAZI TU
 
https://rucuso.blogspot.com/2016/04/jpm-vimilia-nilalapo-mbele-na-wewe-hapa.html
VIONGOZI serikalini wakiwemo mawaziri  na makatibu wakuu, wameombwa na Rais John Magufuli, kuvumilia machungu  wakati wa uongozi wake, kama ambavyo wananchi walivyovumilia tangu  Uhuru.
Amesema hayo jana wakati akiweka jiwe  la msingi la ujenzi wa barabara ya kwanza ya juu (flyover) nchini  Tanzania, inayojengwa katika makutano ya Barabara ya Mandela na Barabara  ya Nyerere, eneo la Tazara, kwa ufadhili wa Serikali ya Japan.  Machungu  hayo kwa mujibu wa Rais Magufuli, yataanza kuonekana wakati wa  utekelezaji wa Bajeti ya Serikali ya kwanza kwa Awamu ya Tano, ambayo  fedha za maendeleo zimeongezeka kutoka asilimia 27 za bajeti iliyopita,  hadi kufikia asilimia 40.
Machungu  hayo kwa mujibu wa Rais Magufuli, yataanza kuonekana wakati wa  utekelezaji wa Bajeti ya Serikali ya kwanza kwa Awamu ya Tano, ambayo  fedha za maendeleo zimeongezeka kutoka asilimia 27 za bajeti iliyopita,  hadi kufikia asilimia 40.
Machungu yenyewe Ili kufanikisha  dhamira hiyo ya Serikali, Rais Magufuli alisema katika bajeti hiyo  inayotarajiwa kupelekwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  litakaloanza vikao vyake Dodoma wiki ijayo, machungu hayo yataanza  kuonekana kwani fedha za chai, semina na safari, zimekatwa na kujaziwa  katika fedha za maendeleo.
Kutokana na makato hayo, Dk Magufuli  amesema kutakuwa na machungu hasa kwa watendaji wa Serikali na kuwaomba  mawaziri na makatibu wakuu ambao alisema walikuwa wakifaidi matunda ya  Uhuru, wavumilie machungu hayo kwani wananchi wa maisha ya chini  wamevumilia machungu kwa muda mrefu.
“Wananchi wamechoka kutuona sisi  viongozi tunafaidi matunda ya Uhuru wa nchi tangu Uhuru na wao wakiwa  wasindikizaji halafu wao tunawaomba kura na wakishatupigia tunawasahau,”  alisema na kuongeza kuwa anataka wananchi watoke kwenye machungu na  sasa wawe ‘watamu’ kwa maendeleo.
Magufuli alisema lazima viongozi  wabadilike na kurudi kwa wananchi wa maisha ya chini na hiyo itakuwa  sadaka kwa kuwapa madaraka kwani wananchi wanyonge wameteseka siku  nyingi.
Wasiovumilia Alisema waliokuwa wamezoea  chai, safari na posho za ovyo kama wanaona au wanafikiri hawawezi  kufanya kazi bila hizo chai, waache kazi mara moja kwani sasa fedha  zinazokusanywa za walipa kodi wanyonge, zitaenda kutatua matatizo yao ya  hospitali, barabara na kununua ndege za Serikali.