TORRES AIKUBALI TAJI YA MIBA KWA TIMU YAKE
 
https://rucuso.blogspot.com/2016/04/torres-aikubali-taji-ya-miba-kwa-timu.html

Na Albogast Benjamin
Fernando Torres alianza maisha ya soka  katika jiji la Madrid akiwa na klabu yake ya Atletico De Madrid lakini  dunia ilimtambua zaidi ndani ya miaka minne aliyokaa Liverpool kuanzia  mwaka 2007 hadi 2011.
Baada ya kuhamia Chelsea mambo hayakuwa  mazuri kwake na ilipelekea kuuzwa Inter-Milan kabla ya kutolewa kwa  mkopo kwenye klabu yake ya utotoni ambayo haswa ndio masikani yake  Atletico De Madrid.
Nyumbani ni nyumabni tu kama ambavyo  Gadner G Habash maarufu Captain alivyopokelewa kwa shangwe alivyorejea  Clouds Fm ndivyo ilikuwa kwa Torres alivyo pokelewa vyema nyumbani na  hapo ndo ilikuwa mwanzo wake kuanza kufanya vizuri tena japo kuwa umri  umekwenda.
Kwenye mchezo wa jana wa Uefa hatua ya  robo fainali dhidi ya Barcelona alifunga bao la kuongoza dakika ya 25  lakini ilimchukua dakika kumi baadae akapata kadi nyekundu baada ya  kumchezea rafu kiungo wa Barcelona Sergio Busquet dakika ya 36 hivyo  kuifanya timu yake ifungwe bao 2 – 1.
Kupitia ukurasa wa twitter Torres  amesema haya kuhusiana na kadi hiyo. “I take responsibility for our  defeat, but now more than ever let’s go to The Calderón for a comeback  #ForzaAtleti”